MRATIBU WA ELIMU NA AFYA

on 16th March 2023 by elct

news article

 

 

                         

NAFASI YA KAZI

KKKT- Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria

S.L.P 423 Mwanza

Tel/Fax + 255 282 540 674                                                 

Barua pepe: info@elct-elvd.org

Tovuti: www.elct-elvd.org

Taarifa kuhusu DMZV: Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria ni moja kati ya Dayosisi 27 za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. DMZV inajumuisha mikoa miwili ya Mwanza na Geita.

DIRA YA DMZV: ‘Kuungana katika Kristo ili ufalme wa Mungu utawale.

DHIMA YA DMZV: Kueneza Injili ya Yesu Kristo kwa maneno na matendo kwa watu wote katika mikoa ya Mwanza na Geita na kwingineko.

NAFASI YA KAZI: Mratibu wa Elimu na Afya

IDADI YA NAFASI ZA KAZI: Moja (1)

MAHALI PA KAZI: Ofisi Kuu KKKT-DMZV

ATARIPOTI KWA: Mkuu wa Idara ya Huduma za Jamii

WAJIBU WA KAZI:

·         Kuandaa na kuratibisha vikao vya kikatiba vya vitengo vya Elimu na Afya katika Dayosisi

·         Kubuni njia za uendeshaji wa shule ya Sekondari ya Kilutheri Mwanza na Malya

·         Kushauri uongozi juu ya uendeshaji miradi na program za vitengo vya Elimu na Afya

·         Kusaidia na kuratibisha usajili wa shule za awali na sekondari DMZV

·         Kuratibisha uanzishaji au ufufuaji wa shule za awali au msingi katika sharika

·         Kusimamia utekelezaji wa sera na miongozo mbalimbali ya Elimu na Afya na kuhakikisha kuwa sera na miongozo inasambazwa kwa wadau

·         Kuratibisha utoaji wa ushauri wa Afya kwa wakristo katika sharika za DMZV na kufuatilia uendeshaji wa vituo vya Afya

·         Kuratibisha mradi wa huduma ya mtoto na kijana (compassion) unaotekelezwa katika sharika za DMZV

·         Kubuni na kuandaa miradi ya Elimu na Afya katika Dayosisi

·         Kusimamia watumishi katika vitengo vya Elimu na Afya katika Dayosisi

·         Kufanya kazi zingine zinazopangwa na msimamizi

SIFA ZA MWOMBAJI:

·         Uzoefu katika kazi za huduma za jamii kama vile, Mahusiano ya Umma, Elimu ya Jamii, Uchunguzi wa Afya/Utabibu na maeneo mengine yanayohusiana na maeneo tajwa

·         Uzoefu usipungua mwaka mmoja (1) katika nafasi ya uongozi katika taasisi za Elimu/Afya

·         Uwezo katika kushughulikia masuala ya afya ya umma

·         Mkristo (Mlutheri) na mwenye moyo wa kutumika kanisani

·         Uwezo mzuri wa kuandaa ripoti

·         Ujuzi na uelewa wa kanuni na misingi ya usimamizi wa program za Elimu na Afya

·         Ujuzi wa kutumia kompyuta

·         Ufanisi katika kazi na uwezo wa kufanya kazi Zaidi ya moja.

SIFA ZA KIELIMU:

 

·         Shahada katika fani ya Elimu, Afya ya Uma, Utabibu, Utawala wa Afya (Degree in Health Administration) au fani zingine zinazohusiana katika chuo kinachotambulika na serikali.

 

v  NAMNA YA KUTUMA MAOMBI:

Waombaji wenye sifa wawasilishe Barua za maombi ya kazi, wasifu (CV), Vivuli vya Vyeti na Barua ya Utambulisho kutoka kwa kiongozi wa Dini kwa:

KATIBU MKUU,

KKKT – DAYOSISI MASHARIKI YA ZIWA VICTORIA

S.L.P 423.

BARUA PEPE: elctelvd84@gmail.com  

TAREHE YA TANGAZO: 16/03/2023

MWISHO WA KUTUMA MAOMBI: 05/04/2023                   SAA: 08:00 Mchana

NB: Maombi yawasilishwe kwa njia ya barua pepe tu. Na sio vinginevyo

 

ü  KKKT- DMZV inatoa fursa za ajira kwa watu wote wenye sifa.

 

Mission Statement

ELVD endeavours to spread the gospel of Jesus Christ, through word and deed, to serve all people in the regions of Mwanza, Geita regions.

UPCOMING EVENTS

Jan 26

UZINDUZI RASMI MRADI WA USHIRIKIANO WA UTUNZAJI MAZINGIRA

Friday 08:00 AM

Details →