Nafasi ya Kazi

on 11th March 2023 by elct

news article

NAFASI YA KAZI

KKKT- Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria

S.L.P 423 Mwanza

Tel/Fax + 255 28 2540674                                 

Barua pepe: info@elct-elvd.org

Tovuti: www.elct-elvd.org

Taarifa kuhusu DMZV: Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria ni moja kati ya Dayosisi 27 za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. DMZV inajumuisha mikoa miwili ya Mwanza na Geita.

DIRA YA DMZV: ‘Kuungana katika Kristo ili ufalme wa Mungu utawale.

DHIMA YA DMZV: Kueneza Injili ya Yesu Kristo kwa maneno na matendo kwa watu wote katika mikoa ya Mwanza na Geita na kwingineko.

Taarifa kuhusu Charming Bungalow: Ni nyumba za kulala wageni zinazomilikiwa na KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria, zipo Nyakato karibu na kituo cha Afya/Chuo cha Biblia na Theolojia Nyakato KKKT- DMZV. Uongozi wa Dayosisi unatangaza nafasi moja ya kazi kama ifuatavyo:

NAFASI YA KAZI: Mpishi

IDADI YA NAFASI ZA KAZI: Moja (1)

MAHALI PA KAZI: Nyumba za kulala wageni (Charming Bungalow) - Nyakato

ATARIPOTI KWA: Meneja

WAJIBU WA MPISHI:

·        Kuwajibika katika kuandaa chakula kwa kuzingatia mahitaji ya mteja/mgeni

·        Kuhakisha kuwa chakula na vifaa vyote vya kuandalia chakula vipo katika hali ya usafi na usalama

·        Kuandaa na kupanga mpangilio wa vyakula katika hoteli (Menu)

·        Kufanya usafi eneo la kuandaa chakuala/jiko na mazingira yanayozunguka

·        Kupokea na kushughulikia mahitaji ya chakula ya wageni/wateja

·        Kuwasiliana na wafanyakazi wengine katika kuandaa chakula au kufanya maboresho ya kuvutia kwa wateja

·        Kubuni mapishi mapya katika hoteli

·        Kusimamia na kudumisha mahusiano ya wateja

·        Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wengine namna ya kuandaa chakula

·        Kupokea maoni kutoka kwa wateja/wageni na kuyafanyia kazi

·        Kufanya kazi zingine atakazopangiwa na msimamizi.

 

SIFA ZA MWOMBAJI:

·        Cheti cha usimamizi wa hoteli (Hotel Management)

·        Mwenye cheti cha mafunzo ya utayarishaji wa vyakula mbalimbali vya asili na kigenikutoka katika chuo kinachotambulika atapewa kipaumbele zaidi

·        Uzoefu wa kazi ya upishi katika hoteli au mgahawa/restaurant usiopungua miaka miwili (2) na zaidi

·        Uwezo mzuri wa kuhudumia na kuzungumza na wateja kwa ukarimu (good customer care and hospitality)

·        Mwenye maadili ya Kikristo

·        Mwenye moyo wa kutumika Kanisani

v NAMNA YA KUTUMA MAOMBI:

Waombaji wenye sifa watume Barua za maombi ya kazi, wasifu (CV), Vivuli vya Vyeti na Barua ya Utambulisho kutoka kwa kiongozi wa Dini kwa:

KATIBU MKUU,

KKKT – DAYOSISI MASHARIKI YA ZIWA VICTORIA

S.L.P 423.

AU KWA BARUA PEPE: elctelvd84@gmail.com  

TAREHE YA TANGAZO: 09/03/2023

MWISHO WA KUTUMA MAOMBI: 29/03/2023                   SAA: 08:00 Mchana

 

ü  KKKT- DMZV inatoa fursa za ajira kwa watu wote wenye sifa.

Mission Statement

ELVD endeavours to spread the gospel of Jesus Christ, through word and deed, to serve all people in the regions of Mwanza, Geita regions.

UPCOMING EVENTS

Jan 26

UZINDUZI RASMI MRADI WA USHIRIKIANO WA UTUNZAJI MAZINGIRA

Friday 08:00 AM

Details →