NAFASI YA KAZI
KKKT- Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria
S.L.P 423 Mwanza
Tel/Fax + 255 28 2540674
Barua pepe: info@elct-elvd.org
Tovuti: www.elct-elvd.org
Taarifa kuhusu DMZV: Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria ni moja kati ya Dayosisi 27 za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. DMZV inajumuisha mikoa miwili ya Mwanza na Geita.
DIRA YA DMZV: ‘Kuungana katika Kristo ili ufalme wa Mungu utawale.
DHIMA YA DMZV: Kueneza Injili ya Yesu Kristo kwa maneno na matendo kwa watu wote katika mikoa ya Mwanza, Geita na kwingineko. KKKT-DMZV inamiliki shamba lenye ukubwa wa ekari 1000 katika wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza. Uongozi wa Dayosisi unatangaza nafasi ya kazi moja (1) kwa nafasi ya Meneja wa Shamba:
NAFASI YA KAZI: Meneja wa Shamba (1)
MAHALI PA KAZI: Shamba la Malya - Kwimba
ATARIPOTI KWA: Mkuu wa Idara ya Mipango na Uwekezaji
WAJIBU WA MENEJA WA SHAMBA:
· Kuandaa mpango na ratiba za kilimo, kupanda na kuvuna katika shamba
· Kusimamia na kuhakikisha kuwa watumishi wote katika shamba wana uelewa wa ratiba za kazi
· Kuhakikisha kuwa mbegu, mbolea, dawa za kuulia wadudu na vifaa muhimu vya shamba vinapatikana kwa wakati na kutunzwa vizuri
· Kusimamia na kutunza shamba, mali na miradi iliyopo katika shamba
· Kupokea na kutunza fedha zinazopatikana kupitia shughuli za shamba na kuhakikisha zinahifadhiwa benki na kuepuka kutumia fedha mbichi
· Kudhibiti visumbufu vya mazao na mimea
· Kukusanya takwimu za bei na mazao ya shamba
· Kuandaa taarifa ya utekelezaji ya shamba ya kila miezi mitatu 3, mpango kazi wa mwaka na kuiwasilisha kwa mkuu wa Idara ya mipango na uwekezaji
· Kuhakikisha kuwa uzalishaji wa mazao kwenye kitalu (greenhouse) unafanyika muda wote
· Kutafuta masoko ya bidhaa za shamba na kuhakikisha mazao yanafika sokoni kwa wakati
· Kufanya kazi zingine utakazopangiwa na Mkuu wako wa kazi.
SIFA ZA MWOMBAJI:
· Shahada/Stashahada ya kwanza ya kilimo au shahada ya Sayansi aliyejiimarisha katika mchepuo wa kilimo au fani inayoendana na hiyo kutoka kwenye chuo kinachotambulika na serikali
· Uzoefu usiopungua mwaka mmoja (1) katika kazi.
· Uzoefu wa vitendo katika shamba na ustadi katika uendeshaji na kutunza vifaa/mitambo ya kilimo
· Cheti cha mafunzo katika Kilimo, Uendeshaji wa Mashine, Dawa n.k
· Ujuzi katika matumizi ya kompyuta
· Uzoefu katika Nyanja ya kilimo, uzalishaji wa mazao
· Mkristo mwenye moyo wa kutumika Kanisani
· Ujuzi wa kutumia kompyuta (word, Excel)
· Umri usiozidi miaka 45
· Ufanisi katika kazi na uwezo wa kufanya kazi Zaidi ya moja.
NAMNA YA KUTUMA MAOMBI:
Waombaji wenye sifa watume Barua za Maombi ya kazi, Vivuli vya Vyeti na Barua ya Utambulisho kutoka kwa kiongozi wao wa Dini kwa:
KATIBU MKUU,
KKKT – DAYOSISI MASHARIKI YA ZIWA VICTORIA
S.L.P 423
MWANZA.
KUPITIA BARUA PEPE: elctelvd84@gmail.com
NB: Maombi yatakayowasilishwa kwa njia nyingine tofauti na barua pepe HAYATAPOKELEWA!
TAREHE YA TANGAZO: 16/03/2025
MWISHO WA KUTUMA MAOMBI: Ijumaa Tarehe 04/04/2025 SAA: 04:00 Asubuhi
ü KKKT- DMZV inatoa fursa za ajira kwa watu wote wenye sifa.